Mwanafalsafa maarufu
wa Ufaransa Baron De Montesquieu mtalamu wa Sheria pamoja na masuala ya utawala
katika Ulaya mnamo karne ya kumi na nane aliwahi kuainisha aina tatu za tawala
katika Mataifa,
Aina ya kwanza ni tawala za Kifalme (Monarch) zinazoongozwa na
Wafalme au Malikia, tawala za pili ni zile tawala za Kijamhuri (Republic)
ambazo huongozwa na kiongozi mkuu wa nchi ambaye huchaguliwa na wananchi na
aina ya tatu ni zile tawala za Kiimla au kidikteta (Depotism).
Tanzania
tunaongozwa kwa kutumia Tawala ya Kijamhuri ambapo Rais na Chama Tawala huchaguliwa
kwa kura za Wananchi. Pia tunajiongoza
kwa kutumia Demokrasia ambayo mahali popote Duniani huongozwa na Sheria, na
Serikali huongozwa na Taasisi inayoitwa Dola ambayo inahodhi mamlaka tatu muhimu
Serikali, Bunge na Mahakama. Mihimili hii mitatu inaundwa na Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania ya Mwaka 1977 kuanzia Kipengele cha Pili mpaka cha Sita
ambapo umetolewa ufafanuzi wa kina namna Mihimili hii inavyotakiwa kufanya kazi
kwa uhuru bila kuingiliwa na mwingine kwa manufaa ya umma.
Tanzania pia tunajiongoza kwa kutumia
Demokrasia ambapo kila mwananchi anakuwa na haki ya kusikia na pia kupewa haki
zake zinazolindwa Katiba. Ndio maana Serikali yetu Mwaka 1977 kwa kutumia Katiba
ya Jamhuri Kipengele Namba 129 iliunda rasmi Tume ya Haki za Binadam na Utawala
bora (CHRAGG) kama chombo chake huru cha kulinda haki za wananchi na kusimamia
utawala bora pamoja na kuchunguza malalamiko ya ukiukwaji wa haki za wananchi
na hata kwenda kwenye Sheria inapobidi. Rais wa Tanzania ndiye Amiri Jeshi Mkuu
ambaye moja ya kazi zake ni pamoja na kusimamia vyombo vya Dola na kuhakikisha
Sheria zilizotungwa na Bunge zinatekelezwa kwa mujibu wa Katiba, kwenye
kulitimiza hilo Rais huteuwa wasaidizi wa kumsaidia kwenye kazi hizo. Kwa hiyo
linapotokea tatizo lolote la Kitaifa au Kisiasa linatakiwa kufikishwa aidha
Mahakamani, Bungeni au kwenye Dola, lakini sio mahali popote pengine. Kama ni
tatizo la Vyama vyetu vya siasa Katiba ipo wazi kwamba Msajili wa Vyama vya
saisa atahusishwa namna ya kulimaliza au kuishauri Serikali namna ya kulimaliza
kama kweli lipo tatizo.
Kwa mantiki hii basi kitendo cha Tume ya Haki
za Binadam na Utawala Bora kuwaita Mkuu wa Polisi na Mwanasheria Mkuu hakihalalishwi
mahali popote kwenye Katiba yetu, na hata kuwaita CCM na Chadema waje meza moja
bado sio kazi yao inatakiwa kuwa kazi ya Msajili wa Vyama vya Siasa nchini. Kwa
hiyo kitendo cha CCM, IGP na AG kutohudhuria kikao hicho ni halali kabisa kwa
sababu IGP na AG ni wateule wa Rais au Mhimili wa Dola sasa Dola inaitwaje na
Tume tu ni kichekesho kikubwa sana kwa utawala tunaofuata wa Demokrasia na
mgawanyo wa madaraka kwa Mihimili Mitatu mikuu ya Taifa.Tume ya Haki za Binadam
na Utawala Bora haina mamlaka Kikatiba ya kuwaita wateule wa Rais kwa ajili ya
kuwahoji namna wanavyotekeleza wajibu wao kwaa melekezo ya Kikatiba chini ya
Rais wa Jamhuri. Lakini Tume hiyo inaweza kwende mahakamani au kumshauri Rais
iwapo itaona kuna tatizo la ukiukwaji wa haki za wananchi ambao mpaka sasa
haujatokea bado isipokuwa kuna uvunjwaji mwingi wa sheria ambao umekuwa
ukifanywa na Wapinzani kwa kisingizio cha kubanwa Demokrasia.
Na mwisho ni kwamba hakuna tatizo kama tatizo ambalo
litashindwa kutatulika kwa kukataa kwa CCM, IGP na AG kuhudhuria kikao hicho cha
Tume kuwakutanisha na Chadema, hapana lililopo ni uvunjwaji wa Sheria
unaofanywa na Chadema ambao vyombo vya Dola vimekuwa imara sana kwenye
kuthibiti tatizo hilo. Ninarudia tena kama lipo ni tatizo linalotakiwa
kumalizwa na Sheria, lakini sio mkutano kama huo uliopangwa na Tume ya Haki
ambayo huenda hapa inaweza kuwa imepitiliza mipaka yake ya kikazi Kikatiba.
Iwapo wangekubali kuhudhuria kikao hicho basi Kikatiba ingeleta hata mgogoro wa
Kikatiba kwa sababu ingemaanisha Tume hiyo kuwa juu ya Dola, Bunge na Mahakama
vyombo vitatu vikuu ambavyo pekee tu ndio vina uwezo wa kuwaita wahusika wote hao
lakini sio Tume ya Haki za Binadam na Utawala Bora kwa sababu hawana hayo mamlaka.
By:- William Malecela.
Imechapishwa Gazeti la Jambo Leo Tarehe 16/8/2016 na kila JUMANNE.

0 comments:
Post a Comment