Msanii Diamond Platnumz ametangaza neema kwa vijana ambao wanaweza kuungana na kucheza wimbo wake wa Kidogo ambao ameshirikiana na P Square na kusema kikundi ambacho kitakuwa kimechezwa haswa kitapewa pesa taslimu milioni tano.
Katia ujumbe wake huo Diamond amesisitiza kuwa vijana hao wanatakiwa kuchanga na style zao wenyewe ili tu wanatakiwa kuwa wameua kweli si kitoto ili kushinda pesa hizo
"NIKO na MILIONI 5 Cash Mkononi kwa kikundi kitachotuma clip ya kudance #KIDOGO sawia haswaaaa!!! yani sio kiwasiwasi waue Haswaaaa....... tena wamix na style zao wenyewe... Narudia tena Wauwe haswaaa!!!... haya wapigie simu wanao Mjipange kesho Mtume clip kwa namba hii +255654019091 na mkisha tuma mpandishe insta na kuhashtag neno #KIDOGO .... na kesho hiyo ntatangaza Mshindi Anapatikanaje"


0 comments:
Post a Comment