Posted by Williammalecela.com on Monday, August 01, 2016
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Mkuu wa Mkoa wa Songwe Lt. Mstaafu Chiku Galawa (Kulia) wakati alipotembelea ofisini kwake kupata taarifa ya hali ya miundombinu katika mkoa huo.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akitoa maelekezo kwa Meneja wa wakala wa barabara nchini (Tanroads) mkoa wa Mbeya Eng. Paul Lyakurwa wakati alipokagua barabara ya Ikana-Makamba –Chitete iliyopo mkoa wa Songwe.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa akikagua kituo cha kukuza mawimbi ampilification station kilichopo miangalau mkoani Rukwa. Kulia kwake ni Meneja wa kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) Mkoa wa Katavi na Rukwa Bw. Peter Kaguru.
Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Zelothe Stephen akitoa taarifa ya hali ya Miundombinu katika mkoa huo kwa Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa wakati alipomtembelea ofisini kwake.
0 comments:
Post a Comment