Sunday, December 11, 2016

Kama ujuavyo kuwa hivi sasa hakuna kificho kuwa wasanii Ommy Dimpoz na Alikiba wamekuwa maswahiba hasa baada ya kufanya kazi ya pamoja walioipa jina "KAJIANDAE" kazi hiyo imewafanya wawe karibu zaidi huku hali ya urafiki wake na Diamond Platnumz ukipungua siku hadi siku hadi kufikia kutupiana Vijembe Mtandaoni.
Baada ya Tuzo za EATV ambazo msanii Ommy dimpoz alipanda stejini Kutumbuiza pamoja na Alikiba Wimbo wao wa KAJIANDAE tumeinyaka Video ya Ommy Dimpozi ikimuonesha akimuelekeza alikiba kuwa alikosea wakati wanaimba wimbo huo.
Lakini hali hiyo imetafsiriwa kama ni Kijembe kutokana na Ishara aliyoitoa Msanii huyo wakati alipokuwa akitoa maelekezo kwa swahiba wake Alikiba.

0 comments:

Post a Comment