Tuesday, December 27, 2016

 
Rais wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, ametuma salamu zake za kuufunga mwaka 2016 na kuukaribisha mwaka 2017 kwa watanzania, huku akiwataka kudumisha umoja.

Katika ujumbe wake alioutuma kupitia mtandao wa Twitter, Rais Magufuli amewataka watanzania kuendelea kuulinda na kuudumisha umoja katika mwaka 2017.
"Watanzania wenzangu, tukiwa tunakaribia kuumaliza mwaka 2016, naomba niwatakie heri ya Mwaka Mpya 2017, Ombi langu kwa Watanzania wote tuulinde,tuutunze na kuudumisha umoja wetu ktk mwaka 2017 kwa kufanya kazi kwa bidii. MUNGU IBARIKI TANZANIA."

0 comments:

Post a Comment