Thursday, December 29, 2016

Mfanyakazi wa Vodacom Tanzania,Mosi Nasoro(kulia)akishuhudia Meneja Uhusiano wa kampuni hiyo,Matina Nkurlu akiwaonesha waandishi wa habari(hawapo pichani)namba ya mmoja ya washindi kati ya 50 wa mtandao huo waliojishindia shilingi Milioni 1/-kila mmoja na 26 kujishindia shilingi laki 1 kila mmoja wakati wa droo ya wiki ya tatu(3)ya Promosheni ya”Nogesha Upendo”jijini Dar es Salaam leo.Ili ushinde mteja anatakiwa kujiunga na kifurushi chochote cha mtandao wa Vodacom na kujishindia muda wa maongezi,Vifurushi vya intaneti pamoja na fedha taslimu.Meneja Uhusiano wa Vodacom Tanzania,Matina Nkurlu(kushoto)akifafanua jambo kwa waandishi wa habari(hawapo pichani)wakati wa kuchezesha droo ya wiki ya tatu(3)ya Promosheni ya”Nogesha Upendo”jijini Dar es Salaam leo iliyowafanya wateja 50 wa mtandao huo kujishindia shilingi Milioni 1/-kila mmoja na 26 kujishindia shilingi laki 1 kila mmoja ili kushinda mteja anatakiwa kujiunga na kifurushi chochote cha mtandao wa Vodacom na kujishindia muda wa maongezi,Vifurushi vya intaneti pamoja na fedha taslimu.

0 comments:

Post a Comment