Saturday, December 10, 2016



Kuna tofauti   kati ya wanamuziki hawa wawili ambapo kila mmoja ana udhaifu wake tofauti na mwengine na  ubora wake kuliko mwengine .

Moja ya Toafuti kubwa walizonazo wasanii hawa wawili ni pamoja na mitindo yao ya uwimbaji pamoja na aina ya mashabiki wao
Ali Kiba ni Mshairi ambaye anatumia muda mwingi kuhani akiwa kwenye wimbo wake au wa kushirikishwa lakini Diamond  yeye ni mtu wa kunata na mdundo ambapo yeye hubebana na mdundo na kutengeneza mziki wake.
Diamond ni Mfanyabiasaha mzuri kuliko Ali Kiba analijua vizuri soko lake na hawezi kuyumba kwa sababu tayari amejitengenezea soko kubwa ambapo yeye mwenye alishawahi kukiri kwenye vyombo vya habari kuwa yeye hauzi audio yeye anauza videos kwa kughalamika sana kwwenye videos na kufanya videos zenye ubora wa hali ya juu. Ali Kiba yeye ni  sio mtu anayejua vizuri soko hapo ndipo napoonekana kana kwamba sio mtu mwenye mafanikio kwani yeye anajua kuimba nyimbo nzuri lakini hawezi kushawisha watu nje na ndani ya nchi kupenda ngoma zake kwa sababu tu hafanyi uwekezaji mkubwa kwenye videos.
Skendo au Kick amini usiiamini Diamond anaishi kwenye maisha ya  skendo na kick ambapo anapenda kucheza na akili za watu kwenye mitandao ya kijamii kwa kufanya hilo mara lile mara nyingi huwa ni vitu vya kijinga.  Kiba kwenye  masuala ya kick na Skendo yupo mbali sana amabapo kila jambaoa analolifanya huwa na sababu za kufanya hajawi kuweka wazi mahusiano yake zaidi ya watu kumdhania tu ingawa naye anamoenzi wake wala kuonyesha anachofanya akiwa na mpenzi wake fargha kama anavyofanya Diamond.
Kudance  au kucheza kulitawa jukwaani  bila shaka Diamond Platnumz ni dencer nzuri ambapo akiwa jukwaani huwa anacheza kwa mitindo mbalimbali ya kuwafurahisha mashabiki wake tofauti na  Kiba ambaye mara nyingi huonekana  sio nzuri kwenye kudence.

Utunzi ni sifa kubwa sana kwa mwanamuziki kwani mtindo wa mashairi na maneno humthibitisha msanii  Kiba anautunzi bora na mpana kwani anafalsafa yake kwenye jamii akizungumza mambo jamii kama msanii na kuweza kutoa suluhu kwenye nyimbo zake.Diamond huwa mara nyingi hupita kwenye midundo hazingatii sana nini anachowasilisha kwa jamii.    

0 comments:

Post a Comment