Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akizungumza na mtoto mwenye ulemavu wa ngozi katika shule ya msingi Miembeni.
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akimkabidhi mifuko mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa shule ya miembeni, Kuruthumu Hamisi
Picha ya pamoja na ya Naibu Meya na wazazi wa wanafunzi wanaosoma Miembeni shule ya msingi
Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala Omary Kumbilamoto akimkabidhi mifuko mwenyekiti wa kamati ya ujenzi wa shule ya miembeni, Kuruthumu Hamisi
Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii.
Katika kutekeleza sera ya elimu bure Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vingunguti , Omary Kumbilamoto amekabidhi mifuko 12 ya Saruji kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi Miembeni.
Kumbilamoto amesema kuwa mifuko hiyo ya saruji ni kwa ajili ya ujenzi wa sakafu ya madarasa mawili ambayo yamekamilika lakini yalikuwa ayana sakafu.
“mimi nilipita hapa nikafanya ziara na kujionea mapungufu yaliyopo katika ujenzi wa madarasa haya ambayo yalianza kujengwa na kamati ya maendeleo ya shule kwa kushirikiana na wananchi hivyo nimeona nichangie hii mifuko 12 ya Saruji”
Kumbilamoto amewashukuru wananchi waliofika katika hafla hiyo kwani wameweza kujichangisha na kupata shilingi laki mojana ishirini ambazo zitaweza kununulia mchanga wa kujengea.Ametoa wito kwa wadau wengine wa maendeleo kuendelea kumuunga mkono Rais Magufuli kwa kuweza kusaidia maendeleo ya elimu katika kata ya vingunguti.
Kwa upande wake mwalimu mkuu wa shule hiyo Hidaya Hamisi amemshukuru Naibu meya kwa msaada huo ambao utaweza kusaidia kukamilika kwa ujenzi wa madarasa hayo na kuondoa msongamano kwa wanafunzi.
Naibu meya wa Manispaa wa Ilala, Omary Kumbilamoto akikabidhi mifuko ya saruji kwa mwalimu mkuu wa shule ya msingi Miembeni, Hidaya HamisiPicha ya pamoja na ya Naibu Meya na wazazi wa wanafunzi wanaosoma Miembeni shule ya msingi


0 comments:
Post a Comment