Ni kutokana na watumishi wa hospitali kuwatuhumu wafanyakazi wenzao 21 kuwa na VYETI vya KUGUSHI
- Wafanyakazi 10 waliopunguzwa kazi wadai zoezi kikighubikwa na rushwa na upendeleo 

MKUU wa Mkoa wa Mbeya leo ametembelea hospitali teule YA IFISI halmashauri YA Mbeya na kutangaza kuunda Tume YA watu 8 kuchunguza madai mbalimbali YA watumishi wa hospitali hiyo ikiwemo madai YA watumishi 21 wa hospitali hiyo kuwa na vyeti vya Kugushi kupunguzwa kwa wafanyakazi kwa upendeleo na kupunguziwa mishahara kutoka shilingi 320,000 hadi sh 200,000

Madai yote hayo yametolewa na wafanyakazi na wa hospitali hiyo na kwa ukubwa wa tuhuma hizo Mkuu wa Mkoa ametangaza kuunda Kamati ya watu 8 itakayoongozwa na mganga Mkuu wa Mkoa, idara YA usalama, Takukuru , na maafisa 4 watatoka OFISI YA Mkuu wa mkoa
Ameipa Kamati hiyo siku 14 kukamilisha uchunguzi



0 comments:
Post a Comment