Azitaka halmashauri kupanga bajeti kwa kuzingatia ilani YA Chama cha mapinduzi
- Halmashauri zizingatie sheria na taratibu za Fedha ili halmashauri hizo zipate hati safi
Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Amos Makalla amezitaka halmashauri zote mkoani Mbeya kutenga Fedha asilimia 10 YA mapato YA ndani kwa ajili YA mikopo nafuu kwa Vijana na wanawake

Hayo ameyasema Leo kwenye vikao vya kujadili TAARIFA YA mkaguzi na mdhibiti wa hesabu za serikali katika halmashauri za Busokelo na Rungwe

Aidha amewataka watendaji kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria na taratibu za Fedha ili halmashauri hizo zipate hati safi 

Ameelekeza bajeti zote ziandaliwe kwa kuzingatia ilani YA UCHAGUZI YA Ccm kwa kuwa ndicho Chama kilichopata ridhaa YA wananchi





0 comments:
Post a Comment