Thursday, January 26, 2017

Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii 
Msanii wa muziki wa kughani, Mrisho Mpoto amemuinua Rais Dk John Pombe Magufuli mara baada ya kuimba mashairi yenye mvuto na kutoa hamasa kwa watanzania kujenga nchi na kufanya kazi katika serikali hii ya awamu ya tano. 
Mpoto ambaye leo alikuwa mmoja wa watumbuizaji katika shughuli ya uzinduzi wa mradi wa mabasi yaendayo haraka jijini Dar es Salaam na kuimba mashairi ambayo yaliweza kuwafurahisha watanzania na Rais John Pombe Magufuli na kuamua kuinuka kwenye kiti na kwenda kumpongeza wakati akiimba. 
Mara mpoto alipoanza kuimba aliweza kuinua baadhi ya viongozi na kwenda kumtunza na wadau mbalimbali na hatimae kupitia ushiri huo ambao ulimfurahisha Rais Dk John Pombe Magufuli na ujumbe wake wote na kunyanyuka kwenye kiti na kuamua kwenda kumpongeza 

Wimbo huo ambao ulikuwa na maneno yanayosema ,amka tujenge nchi, amka tufanye kazi,na mashairi kadha wa kadha ambayo yanaleta hamasa kwa watanzania nchi nzima. 

Mpoto ambaye alikuwa ameambatana na msanii mahiri hapa nchini banana zoro ambaye alikuwa amesimama katika upande wa uimbaji wa kiitikio.

0 comments:

Post a Comment