Rais wa Marekani anayemaliza muda wake Barack Obama amepata kazi tayari kama Rais wa PlayList ya mtandao mkubwa wa kusikiliza muziki kwa malipo wa Spotify.
Mtandao huu unaongoza kwa huduma ya kusikiliza album na single za wasanii kwa malipo umetoa nafasi hii ya kwazi kwa Rais Obama Jumatatu ya wiki hii kuwa rais huyu anaweza kuwa “President of Playlists,”.
Spotify imesema kazi hii inahitaji mtu mwenye uwezo wa Obama aliyeweza kuongoza nchi kubwa kwa miaka nane au zaidi.
Mtandao huu wa Spotify ulitaka mtu awe na vigezo kama “Mtu wa kufanya kazi na timu, roho nzuri, mpiga kazi mzuri, rafiki wa watu na awe ameshinda tuzo ya Nobel Peace Prize.”
CEO wa kampuni hii ya Sweden Daniel Ek ametoa offer hii twitter baada ya Obama kusikika akitania kuwa atafanya kazi Spotify.
0 comments:
Post a Comment