Kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na mkuu wa wafanyikazi wa rais huyo wa 41 wa nchi hiyo, Jean Becker kwa sasa hali yake inaendelea vizuri na kuna uwezekano mkubwa akaruhusiwa kutoka hospitalini siku chache zijazo.
Siku chache zilizopita mtoto wake George W. Bush ambaye na yeye aliwahi kuwa Rais Marekani alitoa ripoti kuwa atahudhuria sherehe za kuapishwa Donald Trump huku akiongeza kuwa baba yake, George H.W., hatohudhuria kutokana na umri wake kuwa umeenda sana.
0 comments:
Post a Comment