Klabu ya soka ya Arsenal
inamtihani wa kuhakikisha inaska matokeo katika mchezo wa ugenini dhidi ya
miamba wa soka nchini Ujerumani, klabu ya Beyern Munich.
Kuelekea katika mchezo huo
Meneja wa klabu ya Beyern Carlo Ancelotti, amesema ili kushinda katika mchezo
wa ligi ya mabingwa ni lazima kujitoa na uwe na bahati pia.
Ancelotti amesema kikosi chake
kitahakikisha kinamiliki mpira na kutokuruhusu kufungwa bao.
Nae meneja wa klabu ya Arsenal, kikosi chake kitaingia
katika mchezo wa leo kikiwa kimesahau michezo iliyopita kwani jambo kubwa
lililopo mbele yao ni kuhakikisha wanapata matokeo.
Wenger amesema klabu yake ina faida kubwa kwani imeanzia
ugenini na itamalizia nyumbani.
Katika hatua nyingine Wenger
amesema anawaheshimu sana Bayern lakini ni lazima kikosi chake kipambane ili kiweze kupata
matokeo.

0 comments:
Post a Comment