Thursday, February 9, 2017



Mchezaji wa klabu ya Leicester City, Andy King akiiandikia klabu yake bao la kwanza.

Hatimae klabu ya soka ya Leicester City imefanikiwa kupata ushindi wake wakwanza ndani ya mwaka 2017 ni mara baada ya kuibamiza Derby County kwa kichapo cha mabao 3-1.


Katika mchezo huo wa raundi ya nne katika FA Cup uliopigwa katika dimba la King Power Stadium Leicester ilipata bao la kwanza katika dakika ya 47 mfungaji akiwa ni Andy King.

Mara baada ya bao hilo kupatikana Derby Contry ilipambana na kusawazisha bao hilo katika dakika ya 61 mfungaji akiwa ni Abdoul Razzagui.


Mabao mengine ya klabu ya Leicester City yalipachikwa na Onyinye Ndidi na Damarai Gray. Mabao hayo yalipatikana katika dakika za nyongeza mara baada ya mchezo huo kulazimika kufika katika dakika 120.

Sasa Leicester itashuka tena dimbani February 18 kukipiga dhidi ya Millwall  katika hatua ya 16 bora.

0 comments:

Post a Comment