Thursday, February 23, 2017




Source: Jamii Forum

Kupitia clip ya mazungumzo ya sauti iliyovuja kati ya mama Wema Sepetu na Steve Nyerere mambo mbalimbali yajulikana ambayo ni pamoja na mbinu kadhaa zilizofanyika ili kumuokoa Wema Sepetu na janga zima la dawa za kulevya.


 kutokana na clip hiyo inaeleza kuwa Bw, Steve Nyerere, ndiye mtu aliyefanya jitihada kubwa zaidi kumuokoa Wema Sepetu ikiwemo ni pamoja na kwenda bungeni mjini Dododma ili kuzungumza na baadhi ya viongozi wakiwemo, Mwigulu Nchemba, ambae ni waziri wa mambo ya ndani, mbunge wa geita mjini alimaarufu kama Msukuma, waziri wa sanaa na Michezo, Mhe, Nape Nauye, makamu wa rais mama Samia Suluhu Hassani pamoja na wengine wengi aliowaorodhesha katika mazungumzo yake hayo. 

steve anasema kuwa Nape na kundi lake walipanga kumpigania Wema pasipo yeye kujua kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kuepuka uropokaji wa Wema kwani hawezi kutunza siri.



1. Steve Nyerere ndiye aliyewapa Mwigullu, Nape, Msukuma na Mlinga namba za simu za Mama Wema Sepetu

2. Nape na kundi lake waliapa kupambana na Makonda bila kumshirikisha Wema kwa vile ni mropojaji , angeweza kutoa siri. Lakini siyo siri tena.

3. Nape walifikiri kufanya hivyo ni kumuokoa Wema kwa vile alikitetea Chama wakati wa uchaguzi. Wakasahau kuwa wanakidhalilisha Chama kutetea wauza Unga tofauti na ilani ya Chama inavyosema

4. Kwa upande wake Steve Nyerere alijua akimuokoa Wema, CCM wangerudi kumbembeleza Wema kupitia kwake na hivyo angepiga pesa za kutosha


5. Steve Nyerere aliwafikia pia Wabunge wa CHADEMA wakiwemo Freeman Mbowe na Zitto Kabwe ndiyo maana Bunge lilipuka







Attached Files:

0 comments:

Post a Comment