Shaw, amelazimika kutundika daluga kutokana na kashfa ya
kubashiri matokeo ya mchezo wa kombe la FA ulioikutanisha klabu yake ya Sutton
United dhidi ya Arsenal.
Mchezo huo ulikamilika kwa Arsenal kupata ushindi wa mabao
2-0 mabao hayo yakipachikwa na mwanandinga Lucas Perez pamoja na Theo Walcott.
Katika mchezo huo klabu ya Sutton United ilipewa alama 8-1
katika kampuni za ubashiri wa matokeo hivyo kwa kila aliyebashiri matokeo ya
mchezo huo na kuipa ushindi Sutton United, kiwango cha fedha ambacho angeweka
kingezidishwa mara nane.
Siku ya mchezo husika Wayne Shaw alionekana kuwa ni mtu
mwenye pilika pilika za hali ya juu kwani kabla ya mchezo dhidi ya Arsenal
alionekana akikata majani, wakati wa mapumziko alionekana akiwa Bar, katika
kipindi cha pili alionekana akila pizza.
Hata hivyo vitko vyake viliendelea tena asubuhi kwani muda
mchache kabla ya kujiuzulu alionekana katika mahojiano na kipindi cha
Goodmorning Britain, kabla ya kukamatwa na polisi kwaajili ya kesi ya kubeti
wakati yeye ni mchezaji majira ya saa saba mchana (13:00).
Ilipofika saa tisa na dakika arobaini na tano (15:45) akatangaza kustaafu kucheza
soka.
0 comments:
Post a Comment