Woods, 41, ameyasema hayo ikiwa ni
siku chache toka alipolazimika kujitoa katika michuano ya jangwani huko Dubai, Dubai
Desert Classic katika hatua ya pili ya michuano hiyo kutokana na maumivu ya
mgongo.
Hili ni pigo kubwa kwa Tiger Woods
kwani alirejea uwanjani mwezi December akitokea kuuguza majeraha ya muda mrefu.
Tiger Woods amesema mara baada ya
kukaa nje ya mchezo wa gofu kwa miezi 15 aliamini kwamba angerejea rasmi katika
mchezo huo na kupambana ili kurejesha heshima aliyokuwa amejizolea siku za
nyuma.
Kutoka mwaka 2015 hadi sasa Tiger Woods
hajafanikiwa kutwaa taji lolote na katika michuano kadhaa aliyoshiriki amekwa
akipata matokeo mabaya.
Katika michuano ya Hero World iliyoshirikisha
wachezaji 18 wa mchezo wa gofu, Tiger woods alimaliza katika nafasi ya 15
kati ya watu 18 kwenye michuano ambayo ilifanyika huko Bahamas.


0 comments:
Post a Comment