Wednesday, February 1, 2017

Kila mtu alilipokea kwa style yake hili suala la mtayarishaji na msanii mkubwa wa muziki barani Afrika Don Jazzy kujirecord video akiimba wimbo wa Chura wakwake Snura.

Wapo ambao walilichukulia kama kawaida tu, ila pia wapo ambao walilichukulia kama hatua kwa muziki wa Bongo Fleva, na hivyo kitendo hicho kuwa kama surprise kwa wengi.
Perfect255 imepiga story na Snura kujua vipi alikipokea kitendo hicho. Snura ametusanua kuwa sio mara ya kwanza kwa Don Jazzy kufanya hivyo, bali alikwisha wahi kupost clip ambayo Snura na team yake walikuwa wakicheza wimbo huo huo wa Chura. Na hivyo ni dhahiri kabisa kwamba mkali huyo wa Mavin anauzimia wimbo huo wa Chura.
Snura hajataka kupoteza wakati wala nafasi, ameamua kutembelea chaki kwa kuuachia uongozi wake kazi ya kutafuta connection na mwisho wa siku kufanya kazi na Don Jazzy kwakuwa anaamini kuwa Don Jazzy ni shabiki wake.
Play hii video hapa chini kumsikiliza Snura alivyokuwa akipiga story na Perfect255.

0 comments:

Post a Comment