Friday, February 10, 2017


Mwanadada Maria Sharapova amepata mwaliko wa kushiriki katika michuano ya wazi ya Madrid ikiwa yamesalia majuma mawili kabla hajamaliza adhabu yake ya kukaa nje ya uwanja kwa miezi 15.


Sharapova alifungiwa mara baada ya kubainika kwamba ametumia dawa aina ya meldonium, dawa ambayo imepigwa marufuku kutumika michezoni.

Mara baada ya kupewa kadi ya mwaliko wa kushiriki ni wazi sasa Sharapova ataonekana tena katika ulimwengu wa mchezo wa tennis tarehe 5 ya mwezi May.

Mratibu wa tamasha hilo Manolo Santana amesema wamelazimika kumualika Sharapova kwani alionesha nia ya kutaka kushiriki katika michuano hiyo.

Manola amesema Sharapova amekuwa mchezaji bora kwa zaidi ya miaka 15 lakini pia amekuwa akifanya vema katika michuano ya wazi ya Madrid kutokana na uwezo alionao.

0 comments:

Post a Comment