Kocha wa
mwanariadha Mo Farah, Alberto
Salazar amekanusha vikali taarifa za kwamba anarudidha nyuma jitihada za kupiga
vita dawa zilizokatazwa michezoni.
Alberto Salazar raia wa Marekani amekuwa
chini ya upelelezi maalum kutoka mwkaa 2015 mara baada ya kipindi cha BBC
Panorama kkumhusisha na kashfa ya kuwasaidia baadhi ya wanariadha kupata dawa
zinazosisimua misuli katika kambi ya wachezaji wa Marekani.
Kwa mujibu wa ripoti iliyovuja
ilieleza kwamba Salazar alimpatia mwanariadha Mo Farah pamoja na wanariadha
wengine dawa za kusisimua misuli aina ya L-carnitine.
Licha ya kushukiwa na kujihusisha
huko, Alberto amesema anaamini katika mchezo ulio msafi, pamoja na mazoezi ya
kutosha na haungi mkono matumizi ya dawa zilizokatazwa michezoni na anaunga
mkono juhudi za Wada pamoja na IAAF.
![]() |
| Mwanariadha Mo Farah |
Kocha huyo amesema katika
kuonyesha namna anavyounga mkono jitihada za WADA amewasiliana na USADA na
amekuwa akijitolea kutoa ushirikiano wa kutosha.
Katika michezo ya Olimpiki ya mwaka 2016
iliyofanyika nchini Brazil, Mo Farah alikuwa mwanariadha wa kwanza kutoka
nchini Uingereza wa mbio na uwanjani kushinda medali tatu za dhahabu katika mbio
za mita 10,000 mjini Rio.
Mo Farah alijikwaa wakati wa mbio hizo, lakini
aliinuka na kujikaza vilivyo katika mita 100 za mwisho na kushinda kwa muda wa
dakika 27 sekunde 5.


0 comments:
Post a Comment