Shirikisho la Riadha Tanzania (RT),
limekamilisha hatua ya kwanza na ya muhimu ya maandalizi ya kuelekea Mashindano
ya Dunia ya Mbio za Nyika ‘World Cross Country’ zitakazofanyika Kampala Uganda
Machi 26, Mwaka huu.
Jumamosi, Februari 18 RT iliendesha Mashindano
ya Taifa ya Mbio za Nyika katika Viwanja vya Gofu mjini Moshi mkoani
Kilimanjaro na kushirikisha mikoa zaidi ya 11 Tanzania Bara na Visiwani, ambapo
wakongwe wengi wa riadha wamekiri kwamba mwamko waliouona juzi haujatokea tangu
mwaka 1991 kwenye mashindano yaliyofanyika Arusha eneo la Mushono.
Mwaka huo wa 1991, ndiyo mwaka ambao
mtanzania pekee Andrew Sambu alishinda mashindano ya Junior ya Dunia Antwerp
Belgium, kwa mfano huo sisi Shirikisho la Riadha Tanzania tuna imani kubwa na
timu iliyochaguliwa mwaka huu, tunakwenda Uganda kifua mbele, hatuogopi
chochote, mataifa mengine nayo yanafahamu kwamba watanzania wameamua safari
hii.
Majina ya wanariadha waliochaguliwa
kwenda kusaka medali Uganda na kupeperusha vyema bendera yetu.
Waliochaguliwa kwenye timu ya Taifa
kwenda Kampala ni wafuatao:
Wanaume Senior 10KM;
1)
Emmanuel Giniki – Manyara
2) Basil
John – CCP / Kilimanjaro
3) Gabriel
Geay – JKT / Arusha
4) Fabian
Joseph – Arusha
5)
Wilbado Peter – CCP / Kilimanjaro
6)
Josephat Joshua – CCP / Kilimanjaro
Wanawake Senior 10KM;
1)
Magdalena Shauri – JKT / Arusha
2)
Angelina Tsere – JKT / Arusha
3) Failuna
Abdi – Arusha
4) Sara
Ramadhani – Arusha
5)
Jackline Sakilu – JWTZ / Arusha
6) Siata
Kalinga – JWTZ / Arusha
Wanaume Junior 8KM;
1)
Francis Dambel – Manyara
2) Yohana
Elisante – JKT / Arusha
3)
Ramadhani Juma – Arusha
4) Elisha
Wema – Arusha
5)
Anthony Wema – Arusha
6)
Joshua Elisante – Arusha
Wanawake Junior 6KM;
1)
Cecilia Ginoka – JKT / Arusha
2)
Maicelina Issa – JKT / Arusha
3) Asha
Salum – JKT / Arusha
4) Noela
Remy – Manyara
5)
Elizabeth Boniface – Singida
6) Amina
Mgoo – JKT / Arusha
Timu ya Relay Wanaume wawili;
1) Faraja
Damas – JKT / Arusha
2) Marco
Sylvester – Singida
Timu ya Relay Wanawake wawili,
itangazwa hivi karibuni kutokana na sababu za kiufundi.
Makocha wa timu ya taifa;
Kamati ya Ufundi ya RT, imewapendekeza
wafuatao kuwa makocha wa timu hii ya Taifa.
1) Naasi
Gwagwe Dengwe – CCP
2) Thomas
John Tlanka– Arusha
3)
Francis Nade – Manyara
4)
Zakaria Barie – Arusha
5) Lwiza
John - Mbeya

0 comments:
Post a Comment