Wachezaji
wa mchezo wa bao kutoka katika klabu ya Sisi kwa Sisi yenye maskani yake
Manzese jijini Dar es Salaam wapo katika mazoezi makali wakijiandaa kwaajili ya
mchezo wa mardiano dhidi ya klabu ya Kizota ya Mburahati.
Katika
mahojiano na Blogu ya Wananchi mmoja wa wachezaji wa Sisi kwa Sisi
Thomson Kauchungu amesema timu yake ilipoteza katika mchezo wa awali kwa
kukubali kichapo toka Kizota hivyo sasa wanataka kufuta uteja.
Nae
mwenyekiti wa sisi kwa sisi Mzee Mohamed Mkumba amewataka wadau na mashabiki wa
kizota wajiandae kupokea kipigo kikali kwani wachezaji wa klabu yake
wamejipanga vya kutosha.
Mkumba
amesema wachezaji wa sisi kwa sisi wamekuwa wakifanya mazoezi ya mara kwa mara
ili kuimarisha viwango vyao.
Katika
hatua nyungine Rais wa Shirikisho la mchezo wa bao nchini Shibata Monday
Likwepa amesema mchezo huo utakuwa ni wa kusisimua kutokana na upinzani uliopo
pamoja na viwango vya wachezaji toka katika vilabu vyote viwili.

0 comments:
Post a Comment