Friday, February 10, 2017


Klabu ya Azam FC, inataraji kushuka dimbani siku ya kesho kuwakabili maafande wa Ruvu Shooting, katika mchezo utakaopigwa katika Uwanja wa Mabatini uliopo Mlandizi mkoani Pwani.

Kocha Msaidizi wa Azam FC, Idd Nassor Cheche, amesema kuwa kikosi chake kinakwenda Mabatini kuendeleza wimbi lao la ushindi kwa kuichapa Ruvu Shooting.

Cheche amesema wanandinga wa Azam FC wapo katika morali kubwa ya kufanya vizuri kwenye mchezo huo kutokana na mazoezi makali wanayopewa chini ya benchi la ufundi linaloongozwa na Mromania, Aristica Cioaba, pamoja na wasaidizi Msaidizi wake, Idd Cheche na Kocha Makipa, Idd Abubakar.

0 comments:

Post a Comment