Thursday, February 16, 2017

Image may contain: 1 person, sunglasses
Serikali kupitia Baraza la sanaa la Taifa (BASATA) imeufungia wimbo wa Nikki Mbishi wa "I AM SORRY JK" kwa madai kuwa maudhui ya wimbo huo ni kinyume na maadili.
Kufuatia katazo hilo, serikali imepiga marufuku wimbo huo kuchezwa katika chombo chochote cha habari na katika maeneo ya umma. Pia mtu (binafsi) atakayekamatwa anausikiliza wimbo huo (nyumbani, kwenye gari etc) atachukuliwa hatua za kisheria.
Uamuzi huo umekuja saa chache baada ya rapper huyo kuitwa na Baraza la Sanaa la Taifa, BASATA Jumatano hii kujielezea kuhusiana na wimbo huo. Kupitia Instagram, Nikki amewaonya watu kuusambaza wimbo huo kwakuwa mkono wa sheria utawaangukia.
“Naomba niombe radhi kwa vyombo vyote vya habari kuwa sitoweza kuwapa ushirikiano wowote kuhusu wimbo wangu wa “I’M SORRY JK” uliositishwa na hii ni kwa usalama wao na wangu pia,” ameandika Nikki kwenye Instagram.

0 comments:

Post a Comment