Tuesday, March 14, 2017


Afrika kusini imeenguliwa katika uenyeji wa wa michezo ya jumuiya ya madola yaani Commonwealth iliyokuwa imepangwa kufanyika katika jiji la Durban 2022.


Akitaja sababu ya Jiji la Durban kutohodhi tena michezo hiyo, Mkurugenzi mkuu wa michezo hiyo David Grevemberg, amesema jiji hilo limeshindwa kufikia vigezo na masharti waliyokuwa wamepewa.

Mapema mwezi uliopita waziri wa Michezo wa Afrika Kusini Fikile Mbalula alisema michuano hiyo isingeweza kufanyika nchini Afrika Kusini kutokana na matatizo ya kiuchumi.
Waziri Fikile alisema serikali ya Afrika Kusini ilijitahidi kuhakikisha maandalizi hayo yanakamilika kwa wakati lakini Serikali haina fedha hivyo hawawezi kuandaa tena michezo hiyo.

Katika hatua nyingine Waziri huyo amesema kutokana na ukata huo wameona ni vema wkaiacha serikali itatue kwanza changamoto zinazoikabili  ikiwa ni pamoja na kutatua changamoto zinazowakabili wananchi wa Afrika kusini.

Durban ilipewa nafasi ya kuandaa michezo hiyo mwezi September 2015 na kama michezo hiyo ingefanyika ingekuwa ni mara ya kwanza kwa michezo hiyo iliyoanza mwka 1930 kufanyika barani Afrika.

Sasa miji ya Liverpool na Birmingham ndio ambayo imeonyesha nia ya kutaka kuhodhi michezo hiyo inayotaraji kufanyika 2022.

Msemaji wa jii la Liverpool ndie ambae amethibitisha kwamba jiji hilo linaweza kutumika kama mweyeji wa michuano hiyo.

Kwa upande wa jiji la Birmingham maandalizi ya michezo ya jumuiya ya madola ya mwaka 2026 yameshaanza hivyo Diwani wa jiji hilo Ian Ward, amesema wanaweza kuwa wenyeji wa michezo ya mwka 2022 pia.

Ian amesema tayari miundombinu ya miichezo mbalimbali imeshaanza kutengenezwa hivyo jiji hilo halitakuwa na kazi kubwa katika maandalizi ya 2022.

Atakaepata fursa ya kuhodhi michuano hiyo atatangazwa mwishoni mwa mwaka huu.


Michezo ya jumuiya ya madola hufanyika kila baada ya miaka mine ikishirikisha wanamichezo wa michezo mbalimbali toka katika mataifa 50 ambayo yameshawahi kuwa makoloni ya Uingereza.

0 comments:

Post a Comment