Wednesday, March 22, 2017


Bondia Anthony Crolla amesema anaamini ubinafsi na moyo wa kujiona kwamba yeye ni bora ndio utakaofanya pambano lake la siku ya jumamosi katika jiji la Manchestter liwe la kuvutia sana.

Anthony atashuka ulingoni siku ya jumamosi kuzichala dhidi ya bondia Jorge Linares ambae ni bingwa wa WBA.

Hii itakuwa ni mara yake yakwanza kushuka ulingoni ndani ya miezi sita toka alipozichapa dhidi ya bondia Jorge Linares katika ukumbi wa Manchester Arena.

Akizungumzia maandalizi yake kuelekea katika pambano hilo, Anthony amesema kasi yake imeongezeka na amekuwa na ufanisi wa hali ya juu, na amekuwa akifanya mazoezi mazoezi akiwa mafichoni.

Kocha wa Anthony Joe Gallagher ndio ambae amemwambia bondia wake aw mbinafsi na mwenye hasira ili aweze kupata ushindi katika pambano hilo.

Pambano hilo linatazamiwa kuwa zuri na lenye kuvutia kwani mpinzani  wa Anthony anasifika kwa kuwa na makonde mazito akitumia mikono yake yote miwili.

Kutokana na ubora wa mpinzani wkae Anthony amesema anafahamu pambano huwa gumu pale bondia mmoja anapokutana na bondia mwingine ambae ni mzuri kwa kiwango lakini kwake ni lazima aufanye usiku wa pambano hilo katika jiji la Manchester uwe usiku mzuri kwake.

0 comments:

Post a Comment