Monday, March 6, 2017


Meneja wa klabu ya Manchester City Pep Guardiola amesema ni vigumu sana kuizuia klabu ya Chelsea isibebe taji l;a ligi kuu soka nchini Uingereza msimu huu.


Pep Guardiola ameyasema hayo mara baada ya kukamilika kwa mchezo ulioikutanisha klabu yake dhidi ya Sunderland na kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Kwa sasa klabu ya Chelsea inaongoza katika msimamo wa ligi kuu soka nchini Uingereza ikiwa na jumla ya alama 63 na mchezo mmoja mkononi dhidi ya West ham United.

Klabu inayoifata Chelsea kwa karibu ni klabu ya Tottenham ikiwa nyuma kwa alama 7 na sasa itakutana na Stoke siku ya jumatano.


Guardiola amesema tofauti ya alama ni kubwa sna na Chelsea nayo imekuwa ikifanya kazi kubwa kila inaposhuka dimbani kwani haizuiliki hata kidogo.

0 comments:

Post a Comment