Uongozi
wa klabu ya Azam umeapa kutokuchukua hatua zozote ikiwemo ya kuandika barua
kwenda katika shirikisho la mchezo wa soka barani Africa CAF kuhusu vurugu walizofanyiwa
nchini Swaziland walipokwenda kukipiga katika mchezo wa mkondo wa pili dhidi ya
klabu ya Mbabane Swalows kwani msimamizi wa mchezo huo alishuhudia vurugu zote
ambazo Azam FC walifanyiwa.
Akizungumza
na Mbungi ya Afrika Swahili TV Afis habari wa Azam FC JAphary Iddy Maganga
amesema kilichowapeleka Swaziland ilikuwa ni kutafuta matokeo ya uwanjani na
kkukiri kwamba wapinzani wao walikuwa wazuri kuwazidi.
Katika
mchezo huo Azam FC walizuiwa kuingia na basi lao uwanjani, lakini pia
wakalazimika kubadilishia nguo katika basi hilo kwani katika chumba chao cha
kubadilishia nguo kulikuwa na hewa nzito sana, hali iliyoashiria kwamba kuna
hewa Fulani ambayo ilipulizwa katika chumba hicho ili kuwachosha wanandinga wa
Azam.
Japha
Iddy amekiri kwamba changamoto ya kukabiliwa na majeruhi wengi imechangia pia
kupoteza katika mchezo huo.
Wakati
huo huo Japha amesema kikosi cha Azam kinataraji kuanza mazoezi yake siku ya
Alhamisi tayari kwaajili ya mchezo dhidi ya klabu ya Yanga utakaopigwa April
mosi katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.
Klabu
ya Azam kwa sasa haipo katika mbio za kuwania ubingwa wa EPL lakini Japha
ameahidi kwamba mpango wa kocha wa klabu hiyo ni kuhakikisha anapata matokeo
katika michezo yote iliyosalia pamoja na kutwaa taji la Kombe la Shirikisho na
hatimae iweze kupata nafasi ya kushiriki katika michuano ya kimataifa msimu
ujao.
0 comments:
Post a Comment