Vilabu vya
soka nchini China vimetumia jumla ya paundi 331 milioni kwa kuzinasa saini za
wanandinga mbalimbali wakiwemo wale waliokipiga katika ligi kuu soka nchini
Uingereza hadi kufungwa kwa dirisha la usajili wakati wa majira ya joto.
Dirisha la usajili nchini China
limefungwa usiku wa February 28 na kuzishuhudia klabu 16 zinazoshiriki katika Chinese
Super League zikigonga hodi katika vilabu mbali mbali nchini Uingereza.
Mwanandinga wa zamani wa klabu ya
Chelsea, Oscar
amejiunga na Shanghai SIPG kwa dau la £60 milioni huku klabu ya
Shanghai Shenhua ikimnasa Carlos Tevez kwa dau la £40 .
Kwa mujibu wa sharia zilizopo
nchini China, wachezaji watatu tu wa kigeni ndio watakaoruhusiwa kuanza katika
mchezo mmoja.


0 comments:
Post a Comment