Wednesday, March 8, 2017


Timu ya Uingereza katika mchezo wa Cricket itakutana na India katika mashindano ya Kombe la dunia katika mchezo huo ICC kwa wanawake huko Uingereza pamoja na Wales.


Mchezo wa ufunguzi kwa Uingereza utakuwa June 24 huku mabingwa watetezi wa taji hilo timu ya Australia wakikipiga dhidi ya West Indies huko Taunton June 26.

Uingereza inashika nafasi ya pili kwa ubora duniani na mchezo wao mgumu utakuwa ni mchezo wa July 9 dhidi ya Australia in Bristol on 9 July.

Timu nane zinazoshiriki katika mashindano hayo zitakutana kwa nyakati tofauti tofauti na baadae timu nne za juu kuingia katika hatua ya nusu fainali na baadae fainali. Itakayopigwa tarehe 23 July

Mataifa yote yatakaoingia katika fainali hizo ni pamoja na Australia, Uingereza, New Zealand, pamoja na West Indies.
Mataifa mengine ni pamoja na Afrika Kusini, India, Sri Lanka pamoja na Pakistan.

Mtendaji mkuu wa ICC David Richardson, amesema hadi sasa tayari zaidi ya tiketi 9,000 za mchezo wa fainali zimeshanunuliwa.


David amesema wanatarji kwamba michuano hiyo itakuwa mizuri na yenye msisimko wa hali ya juu kwani wachezaji wamejipanga kutafuta ubingwa hivyo upinzani utakuwa wa hali ya juu.

0 comments:

Post a Comment