Wednesday, March 29, 2017


Mabondia nchini Tanzania wameaswa kuwa na utamaduni wa kupima afya zao mara kwa mara ili kujua kama kuna matatizo yanayowakabili ili waweze kuepukana na kadhia mbalimbali ikiwemo kupoteza maisha wanapopanda ulingoni.


Katika mahojiano maalum na Blogu ya jamii Rais wa Shirikisho la Ngumi Afrika Mashariki na Kati Yasin Abdala Amesema ni vema mabondia wakawa na utaratibu huo na kuachana na tabia ya kupima afya zao pale tu wanapokuwa wakitaka kuzipiga katika michezo Fulani.

Yasin amesema toka katika mataifa mbali mbali wamepoteza maisha kutokana na kukabiliwa na matatizo mbalimbali ya kiafya wakati walipokuwa wakizichapa ulingoni.

Akitolea mfano matukio yaliyosababisha vifo vya mabondia kwa hapa Tanzania, Yasin amesema miongoni mwa mabondia waliopoteza maisha wakiwa ulingoni ni  Rajabu mandela ambae alifikwa na mauti wakati akizichapa na Musa Chipota, wengine ni Anthony Ndaki ambae aliwahi kuzichapa dhidi ya Charles Kibondo Mawe kutoka Zambia na kufikwa na mauti akiwa ulingoni kutokana na makonde mazito ambayo alipokea toka kwa mzambia huyo.

“Matukio haya sio kwamba yanapangwa, hutokea kwasababu mabondia wanakuwa wamejiandaa kwa sababu kila mmoja anakuwa anataka ushindi” amesema Yasin.

Yasin amesema kwa upande wa bondia ambaye humpiga mpinzani wake hadi kufa, bondia huyo hujiandikishia rekodi nzuri, lakini matatizo yatamfika kama mpinzani wake alikuwa hajafanyiwa vipimo vya afya ili kubaini kama kweli anaweza kuendelea na mchezo huo.

Wakati huo huo yasin amewataka Mabondi wa tanzia waishi kwa malengo ili waweze kuzifikia ndoto zao.
Yasin amesema mabondia wengi nchini wanapoanza kupata fedha hujiingiza katika starehe, hivyo kujikuta wakitumia fedha nyingi katika mambo yasiyo ya msingi badala ya kutumia fedha hizo kufikia ndoto walizojiwekea.

0 comments:

Post a Comment