Wednesday, March 29, 2017


Watanzania wameombwa kujitoa kwa hali na mali ili kuiwezesha timu ya wachezaji wenye ulemavu katika mchezo wa tennis ili waweze kufanya vema katika michuano ya kombe la Dunia katika mchezo wa Tennis BNP Paribas World Cup itakayofanyika nchini Itala kuanzia Mei mosi hadi Mei saba.


Akizungumza na Mbungi ya Afrika Swahili TV Kocha wa Wachezaji wenye ulemavu Riziki Salum amesema timu hiyo inakabiliwa na ukata wa fedha hali ambayo imepelekea timu hiyo kushindwa kuweka kambi nje ya nchi.


Timu niyo inaendelea na mazoezi katika viwanja vya Gymkana jijini dar es Salaam kwa kufanya mazoezi asubuhi na jioni kutokana na ratiba za wachezaji kubana.

 Riziki amesema tayari jitihada mbalimbali zimeshaanza kufanyika kwa kushirikiana na chama cha mchezo wa tennis TTA ili kuhakikisha zinapatikana fedha pamoja na vifaa mbali mbali kwaajili ya safari ya kuelekea nchini Italia.

Kwa upande wa wachezaji wanaokwenda nchini Italia John Albert Churu amesema amejitoa kufanya mazoezi katika jua na mvua lengo lake likiwa ni kuhakikisha Tanzania inafanya vema katika mchezo huo.

Katika hatua nyingine John amewataka watu wenye ulemavu waachane na tabia ya kuomba mitaani, badala yake wajihusishe na michezo mbalimbali kwani itawawezesha kutoka kimaisha.

Timu ya Tanzania kwa wanaume ndio timu pekee kutoka katika bara la Afrika ndio timu pekee inayokwenda kushiriki katika michuano ya BNP Paribas World Cup.

0 comments:

Post a Comment