Monday, March 13, 2017


Bingwa mtetezi wa michuano ya wazi ya BNP Novak Djokovic ameanza vema kampeni yake ya kutetea ubingwa wake mara baada ya kuibuka na ushindi katika mchezo wake wa kwanza dhidi ya Kyle Edmund.

Katika mchezo huo Djokovic alifanikiwa kupata ushindi wa seti 6-4 7-6 (7-5).
Djokovic alifanikiwa kupata ushindi katika seti ya kwanza dhidi ya Briton (22) ndani ya dakika 42, lakini katika seti ya pili alikumbana na upinzani mkali sana kwani Edmund alifanikiwa kupata matokeo katika michezo mitatu ya mwanzo lakini baadae Djokovic alipambana na kusawazisha matokeo hayo na kupelekea mchezo huo kuingia katika tie-break.
Mara baada ya kupata matokeo hayo, sasa Djokovic atakutana na Juan Martin del Potro katika raundi ya tatu mara baada ya Muargentina huyo kupata ushindi katika mchezo dhidi ya Federico Delbonis. Del potro amepata ushindi wa seti 7-6 (7/5) 6-3.
Katika hatua nyingine Roger Federer amefanikiwa kutinga katika hatua ya tatu ya michuano hiyo ni mara baada ya kupata ushindi wa seti 6-2 6-1 tdhidi ya Mfaransa Stephane Robert.
Federer, alifanikiwa kupata ushindi wa asilimia 79 katika mipira aliyoanzisha na hivyo kufanikiwa kushinda ndani ya dakika 52.

Mara baada ya kuvuka katika hatua hiyo, sasa Federer atakutana na Mcheza tennis Steve Johnson. Steve anakutana na Federer kufuatia ushindi wa seti 6-4 3-6 7-6 (7-4) dhidi ya Kevin Anderson toka Afrika Kusini.
Licha ya matokeo ambayo ameyapata, Federer mwanzo wa mchezo wake huo ulikuwa mgumu sana kwake kwani hii ni mara yake ya kwanza kukipiga dhidi ya Steve Johnson.
Nguli mwingine wa mchezo huo Rafael Nadal nae amejikatia tiketi ya kusonga katika mzunguko wa tatu mara baada ya kumshinda Guido Pella na sasa atakutana na Mhispania mwenzake Fernando Verdasco.
Katika michezo yao ya awali Nadal alipata ushindi wa seti 6-3 6-2 huku Verdasco akipata ushindi wa seti 7-6 (7/5) 6-1 dhidi ya Mfaransa Pierre-Hugues Herbert.
Kwa upande wa wanawake Mcheza tenis nambari moja kwa ubora nchini Uingereza Johanna Kontaametupwa nje ya michuano ya wazi ya BNP Paribas mara baada ya kupoteza kwa seti 6-3 3-6 6-7 (1-7) katika mchezo dhidi ya Caroline Garcia.

0 comments:

Post a Comment