Monday, March 6, 2017


Mcheza tennis Jamie Murray pamoja na Bruno Soares wamefanikiwa kutwaa taji lao la kwanza katika michuano ya wazi ya Mexico kwa wachezaji waili wawili.


Katika mchezo huo Jammie pamoja na Bruno walifanikiwa kuwashinda John Isner toka Marekani, pamoja na Mhispania Feliciano Lopez kwa seti 6-3 6-3 huko Acapulco.

Mara baada ya kutwaa taji hilo Jamie amesema ulikuwa ni mchezo mgumu hivyo walilazimika kupambana ili kuupata ushindi huo.

Wakati huo huo Muingereza Andy Murray amefanikiwa kumtandika Fernando Verdasco katika seti mbili mfuflulizo na hivyo kutwaa taji la mabingwa Dubai kwa mara ya kwanza.



Katika mchezo huo Andy Murray alkipata ushindi wa set 6-3 6-2 ndani ya saa moja na dakiak 14.

0 comments:

Post a Comment