Mchezaji nambari moja kwa ubora nchini uingereza Johanna Konta amefanikiwa
kutinga katika hatua ya nusu fainali kunako michuano ya wazi ya Miami ni mara
baada ya kupata ushindi dhidi ya Mromania Simona Halep.
Katika mchezo huo, Konta
alipoteza katika seti ya kwanza kwa 3-6 na baaadae akarejea mchezoni na
kushinda katika seti ya pili kwa 7-6 (9-7) na kasha kupata 6-2 katika seti ya
mwisho.
Mara baada ya kukamilika
kwa mchezo huo Konta amesema ameshukuru sana kwa ushindi alioupata kwani
mpinzani wake alionesha kiwango kizuri na kumpa ushindani mkali sana lakini
sasa anajipanga kwaajili ya mchezo unaofata ambao anaamini utakuwa mgumu zaidi.
Kutokana na matokeo hayo, Konta atakutana na kati ya Venus Williams au Angelique Kerber.
Mchezo mwingine wa
nusu fainali utakuwa ni kati ya Caroline Wozniacki na Karolina Pliskova.
Kwa upande wa wanaume
Fabio Fognini kutoka nchini Italia amemshinda Kei Nishikori kutoka nchini Japankwa
kupata ushindi katika seti mbili za moja kwa moja.
Katika seti ya kwanza
Fabio alipata 6-4 na katika seti ya pili akapata 6-2 na kufanikiwa kuwa
mchezaji wakwanza ambae hayupo katika wachezaji kumi bora kufanikiwa kutinga
katika hatua ya nusu fainali katika michuano ya wazi ya Miami.
Kwa upande wa wachezaji wawili kwa
wanaume, Jamie Murray pamoja na mshirika wake Bruno Soares wametolewa katika
michuano hiyo mara baada ya kupoteza katika seti ya pili kwa 6-3, na seti ya tatu
kwa 10-8, katika seti ya kwanza jammie pamoja na mshirika wake walishinda kwa
6-2.
0 comments:
Post a Comment