Wednesday, March 8, 2017


Bondia Hughie Fury, ambae ni ndugu wa bondia Tyson Fury atapanda ulingoni May 6 mwaka huu kuzichapa dhidi ya bondia Joseph Packer toka nchini New Zealand katika pambano la ubingwa wa dunia WBO uzito wa juu.


Pambano hilo linataraji kuwa kubwa na lenye kuvuta hisia za wengi kwani bondia Parker, 25, amekuwa bondia wa kwanza mzaliwa wa New Zealand-mara baada ya kupata ushindi dhidi ya bondia Andy Ruiz.

Hadi sasa bondia Hughie Fury ameshashuka ulingoni na kushinda katika mapambano 22, kati ya mapambano hayo 18 akiwa ameshinda kwa KO.

Kuelekea katika pambano hilo Fury amesema anamheshimu sana Packer na anafahamu kuwa ni bondia mzuri sana lakini atamshinda katika pambano hilo.

Akimzungumzia ndugu yake Tyson, Fury amesema atahakikisha anashinda katika kila pambano ataloshuka ulingoni ili ndugu yake atakapomaliza kutumikia adhabu yake wajipange kwa pamoja kuuteka ulimwengu wa mchezo wa maumbwi.


Nae mwakilishi wa bondia packer toka katika kampuni ya Duco Events David Higgins amesema mazungomzo yameshafika pazuri baina ya pande zote mbili. 

0 comments:

Post a Comment