Monday, March 13, 2017


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Emil Malinzi kesho amefunga kozi ya ukocha ngazi ya ‘Intermidiate’ kwa makocha 27 waliohitimu kozi hiyo.


Kozi hiyo iliendeshwa na Mkufunzi anayetambuliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF Wilfred Kidao -), katika uwanja wa Michezo wa Bandari, uliopo Tandika jijini Dar es Salaam.

Wakufunzi wengine walikuwa ni Peter Manyika aliyefundisha programu au mtaala kwa makocha wa makipa; Dk. Nassoro Ally Matunzya aliyewanoa makocha hao kuhusu tiba za wanamichezo/wanasoka na Mkufunzi wa muda mrefu wa soka, Hemed Mteza.

Wanafunzi wa kozi hiyo ni Doris Malyaga ambaye ni Mwanamke pekee kati ya wanafunzi 27 walisoma kozi hiyo kwa kipindi cha siku 14 cha mwanzo wa mwaka.

Wengine ni nyota wa zamani wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania ‘Taifa Stars’ waliopata kuchezea klabu kongwe na kubwa nchini. Wanafunzi hao ni Boniface Pawasa, Fred Mbuna, Innocent Haule, Herry Morris, Ivo Mapunda, Nizar Khalfan na Mussa Hassan Mgosi.


Orodha hiyo imewajumuisha pia Omar Kapilima, Amosi Mgisa, Uhuru Mwambungu, Yussuf Macho, George Minja, Haruna Adolf, Selemani Omari, Ally Ruvu, Masoud Selemani, Haji Mustapha, Mhasham Khatib, Issa Ndunje, Salum Kapilima, Said Salum, Julio Elieza, Hassan Mwakami, Rajab Mponda, Ally Mbonde na Evod Mchemba.

0 comments:

Post a Comment