Vitisho hivyo vimetokana na mashabiki kuhisi kwamba Vardy aliushinikiza
uongozi wa Leicester umfute kazi Kocha Claudio Ranieri.
Ranieri alifutwa kazi mwezi Februar, ikiwa ni miezi tisa tu imepita toka
alipoipa Leicester taji la ligi ya Premier nchini Uingereza.
Vardy amesema anasikitishwa sana na vitisho ambavyo amekuwa akivipata kwani
kila kukicha mambo mapya yamekuwa yakijitokeza na kutolea mfano habari
iliyomuhusisha na kukutana na uongozi wa klabu ya Sevilla wakati alipokwenda
kufanyiwa vipimo vya kama anatumia dawa zilizokatazwa michezoni.
Nyota huyo ambae aliiwezesha Leicester kutwaa taji msimu uliopita
amesema muda mwingine alitaka kukaa kimya na kuamini kuwa haya ni mapito tu
lakini alishangazwa na kushtushwa sana wale waliotaka kumfanyia vurugu mke wake
wakati akiwa kwenye gari pamoja na watoto wake.
Shirika la utangazaji la nchini Uingereza BBC limeeleza kwamba baadhi ya
nyota wa klabu hiyo walijaribu kuzungumza na uongozi mara baada ya kukamilika
kwa mchezo dhidi ya Sevilla katika ligi ya mabingwa na kupoteza kwa mabao 2-1
ili kimtetea kocha Claudio Ranieri lakini uongozi wa klabu hiyo haukukubaliana
na mtazamo wa wachezaji hao.
Mara baada ya ranieri kuondoka, mikoba yake ilichukuliwa na aliekuwa
msaidizi wake Craig Shakespeare ambae sasa ataiongoza Leicester hadi mwishoni
mwa msimu.
Katika michezo mine ambayo Shakespeare ameiongoza Leicester hadi sasa
imefanikiwa kupata matokeo katika michezo mine mfululizo na hivyo kusogea hadi
katika nafasi ya 15 katika msimamo wa ligi kuu soka nchini Uingereza pamoja na
ushindi katika ligi ya mabingwa ulioiwezesha kutinga katika hatua ya robo
fainali.
0 comments:
Post a Comment