Wednesday, March 15, 2017


Roger Federer atakutana na Rafael Nadal katika michuano ya wazi ya BNP hatua ya nne, hii ikiwa ni mara ya pili kwa nyota hao kukutana kwa mwaka huu mara baada ya kukutana katika fainali ya michuano ya wazi ya Australia.


Federer amesema amekwenda katika michuano hiyo ili akutane na Rafael Nadal kwani upinzani ambao amekuwa akiupata unamjenga sana na kumfanya awe fiti zaidi.

Katika michuano ya wazi ya BNP Nadal ambae anashikilia nafasi ya tano kwa ubora duniani amefanikiwa kufika katika hatua ya nne mara baada ya kumshinda Mhispania mwenzake Fernando Verdasco kwa seti 6-3 7-5.

Kwa upande wa Mswis Roger Federer, ambae hadi sasa ameshatwaa mataji 18 ya Grand Slam amefanikiwa kufika katika hatua ya nne mara baada ya kumshinda Steve Johnson wa Marekani kwa seti 7-6 7-6.
Nyota mwingine katika mchezo wa tennis Novak Djokovic amefanikiwa kumshinda Juan Martin del Potro.

Mara baada ya Djokovic 6-kupita katika hatua hiyo, sasa atakutana na Nick Kyrgios, toka Australia ambe kwa viwango vya ubora anashika nafasi ya 18.

0 comments:

Post a Comment