Mwendesha
baiskeli Josh Edmondson amesema alikuwa akivunja sharia za mchezo huo kwa
kujichoma kisirisiri sindano ambazo zilikuwa zikijumuisha muunganiko wa vitamin
mbali mbali.
Josh, 24, alikuwa akiitumikia
timu ya Sky mwaka 2013 na 2014, na sasa anakabiliwa na matatizo kutokana na
matumizi makubwa ya dawa za kutuliza maumivu.
Katika mahojiano na Shirika la
Utangazaji nchini Uingereza BBC, Josh amesema mashindano ya mwaka 2014 yalimfanya
akiuke vifungu kadhaa vya UCI kwa mara mbili au tatu ndani ya kila mwezi mmoja.
Mara baada ya Josh kuifichua siri
hiyo, timu ya Sky imesema dawa za kuongeza vitamin zilikutwa katika chumba cha
Josh, lakini hawakuripoti tatizo hilo kwani walihofia kwamba lingekuzwa.
Wakati timu ya Sky ikijitetea kwa
hilo, Josh amesema alikiri kutumia dawa hizo na kuueleza uongozi, lakini
uongozi wa timu hiyo ulifanya kila linalowezekana ili kuyaficha maovu ambayo
yalikuwa yakitendeka.
Dawa hizo zilionekana pia na wachezaji wengine toka katika timu ya Sky
ambao walikuwa wakiishi nae nyumba moja na pia walipiga picha dawa hizo kama
sehemu ya ushahidi.
Mara baada ya kubainika kwamba wachezaji wenzake wameziona dawa hizo,
Josh aliwasiliana na daktari wa timu kwa njia ya Skype ili kuliripoti tatizo
hilo.
Katika mahojiano hayo Josh
alieleza mambo mengine kadha wa kadha ikiwemo:
- Kwenda nchini Italy katika mazoezi ili apate nafasi ya kununua dawa mbalimbali kwaajili ya kuongeza vitamin, dawa ambazo zinaruhusiwa kwa matumizi ya binadamu lakini haziruhusiwi kutumika miongoni mwa wanamichezo.
- Amejihatarishia maisha yake kwa kujisababishia mshtuko wa moyo kwa kujidunga dawa za kuongeza vitamin bila ushauri wa matabibu.
- Alijipa mamlaka ya kununua dawa za kuongeza nguvu mwaka 2013 katika ziara ya Uingereza. Hata hivyo timu ya Sky imejitetea kwa kusema kwamba daktari wa timu ndie aliempatia dawa hizo bila uongozi kujua.
- Hakuweza kutoka katika nyumba yake kwa miezi miwili kutokana na athari za dawa ambazo alikuwa akizitumia kwa wingi.
Katika hatua nyingine Josh amesema alikuwa chini ya msukumo mkubwa mwaka
2014 sio tu kutoka katika timu anayoitumikia, bali hata ndani ya nafsi yake.
Josh amesema alikuwa hataki kuiangusha timu yake wala mashabiki wake
hivyo ilimlazimu kutumia dawa hizo ili aweze pia kuongezwa mkataba.
Sakata la Josh limezidi kuiweka pabaya timu ya Sky kwani mwaka uliopita
mwendesha baiskeli Jonathan Tiernan-Locke alieleza BBC
kwamba alikuwa akipewa dawa za kuongeza nguvu ambazo zimekatazwa michezoni
mwaka 2012 katika mashindano ya kombe la dunia.
Baadae alifungiwa kutojihusisha na mchezo wa baiskeli kwa miaka miwili
mara baada ya kubainika kwamba aalikuwa akitumia dawa zilizokatazwa michezoni
hali iliyompelekea kuamua kujiuzulu.


0 comments:
Post a Comment