Monday, March 27, 2017


Kikosi cha timu ya Taifa ya Vijana wenye umri chini ya miaka 17 Serengeti Boys kimeendelea na mazoezi huko Bukoba mkoani Kagera kikijiandaa kwaajili ya michezo miwili ya kujipima nguvu kalba ya kuelekea katika kambi ya nje ya nchi na baadae kuelekea Gabon katika fainali za Afcon kwa vijana wenye chini ya miaka 17.


Katika mahojiano maalum na Blogu ya Jamii, kocha mkuu wa Serengeti Boys Bakari Shime amesema mazoezi yameendelea vema na anategemea kupata matokeo mazuri katika michezo ya kirafiki.    

Mara baada ya kukipiga katika michezo hiyo miwili Serengeti Boys itarejea jijini Dar es Salaam Aprili 2, na kukipiga dhidi ya Ghana Aprili 3, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam katika mchezo ambao utatanguliwa na hafla ya kuagwa kwa kukabidhiwa bendera.

Kabla ya kwenda Morocco Serengeti boys itaweka kambi ya zaidi ya mwezi mmoja baadaye nchini Cameroon na baadae itakwenda Gabon katika michuano itakayoanza Mei 14, 2017.
Ikiwa Cameroon itacheza mechi mbili za kimataifa dhidi ya wenyejiCameroon kabla ya kwenda kwenye fainali.

Serengeti Boys imepangwa katika Kundi ‘B’ pamoja na mabingwa watetezi Mali, Niger na Angola na endapo itafanikiwa kumaliza katika nafasi mbili za juu katika Kundi hilo itkuwa imekata tiketi ya kushiriki katika fainali za Kombe dunia kwa vijana huko India, Novemba, mwaka huu.

Kikosi cha Serengeti Boys kinaundwa na Makipa:  Ramadhan Kabwili, Samwel Edward na Kelvin Kayego.

Walinzi:  Kibwana Ally Shomari, Nickson Kibabage, Israel Mwenda, Dickson Job, Ally Msengi, Issa Makamba na Enrick Vitalis Nkosi.

Viungo: Kelvin Nashon Naftali, Ally Ng’anzi, Mohamed Rashid, Shaaban Ada, Mathias Juan, Marco Gerald, Abdulhamis Suleiman, Saidi Mussa na Cyprian Benedictor Mtesigwa.


Washambuliaji:  Muhsin Malima Makame, Yohana Mkomola, Ibrahim Abdallah, Assad Juma na Abdul Suleiman.

0 comments:

Post a Comment