Wednesday, March 15, 2017


Timu ya taifa ya Tanzania katika mchezo wa Kriket imeendelea na mazoezi ili kujiweka fiti kuelekea katika mashindano ya mabingwa wa Afrika ICC Afrika Championship ytakayofanyika Afrika kusini.


Kamera ya Mbungi ya Afrika Swahili Tv imewashuhudia baadhi ya wachezaji walioitwa katika timu hiyo wakiendelea na mazoezi ambayo hufanyika asubuhi na jioni.
Timu hiyo inanolewa na Juan Maitre ndio bingwa mtetezi wa michuano hiyo na sasa ina kibarua cha kuhakikisha inatetea taji hilo.

Kabla ya kuanza kwa michuano hiyo Tanzania itacheza kwanza michezo kadhaa ya kirafiki.


Mataifa yatakayoshiriki katika michuano hiyo ni pamoja na Nigeria, Botswana, Zambia, Sieara Leone, Ghana na Tanzania.

0 comments:

Post a Comment