Baada ya kutoka kwa wimbo mpya wa Darassa ‘Hasara Roho‘ na video kali kutoka kwa #Hanscana pamekuwa na baadhi ya kurasa kwenye mitandao ya kijamii zilizojitokeza na kuiponda kazi mpya ya Darassa.
Kupitia IG Yake staa wa Bongo Fleva Baraka Da Prince amemkingia kifua Darassa nakuandika maneno haya MAKALI >>“Tangu nazaliwa sijapata kuona Nchi yenye wajuaji wengi kama #TANZANIA..tangu nazaliwa sijawai kupata kuona Nchi yenye binadamu wenye chuki baada kuona mtu kafanikiwa kama #TANZANIA siku hizi mashabiki wamekuwa walimu wa mashahiri na wamekuwa wajuaji kuliko hata sisi tunaoimba mziki…@Darassacmg katoa wimbo wake mpya… ni wimbo mkali sana sio audio tu..adi video @hanscana_ umeuwa lakini kuna izi page zinazojihita page za udaku siku izi…zinaboa sana naona kuna kitu wanapost sijui waga wanatumiana hili kurudisha mafanikio ya watu nyuma…Ujue mziki sio kitu ki rahisi kama watu wengi humu ndani mnavyodhania na sio lazima kila kitu kiwe sawa au mapokezi kufanana na kilichopita nyuma…Hakuna kitu kinaboa Duniani kama mtu unapoteza muda wako na nguvu nyingi kuwekeza katika kazi yako au kupigania mafanikio yako,alafu kinakuja kijimtu sijui hata kimetoka wapi kinaanza kuponda kile kitu ulichopoteza muda na nguvu nyingi na pesa pia Nyie watu wajuaji mnaboa kinoma…Tungeni zenu Nzuri na video zenu Nzuri tuzione,Hao Hao kesho ndio utawasikia wakiimba kama wimbo wa taifa…. Oy mwanangu @Darassacmg congratulation my brother ngoma kali kinoma tena video ndio umeuwa
0 comments:
Post a Comment