Tuesday, May 2, 2017

Kutoka Bungeni Dodoma leo May 2, 2017, Mbunge wa Kawe Halima Mdee amepewa adhabu ya kusimamishwa kuhudhuria vikao vya Bunge la Bajeti vilivyobaki kuanzia leo. Adhabu hii imetolewa baada Mbunge huyo kutumia lugha ya matusi dhidi ya Spika Job Ndugai na Naibu Waziri wa Afya Hamis Kigwangallah.
Kamati ya Bunge pia imemsamehe Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni, Freeman Mbowe baada ya kukiri kosa la kudharau Mamlaka ya Bunge April 4, 2017. Mbunge mwingine ni Ester Bullaya ambaye amepewa karipio baada ya kukiri kosa lake sawa na Mbowe.

0 comments:

Post a Comment