Thursday, May 11, 2017

Image may contain: 11 people, people sitting and crowd
*10/05/2017 Mkoa wa Pwani.*
Kaimu Katibu Mkuu UVCCM Shaka Hamdu Shaka (MNEC) Leo amendelea na ziara katika Halmashauri ya Wilaya ya Chalinze, kukagua utekelezaji wa ilani, uhai wa CCM na jumuiya zake na kupata taarifa ya maendeleo ya uchaguzi.

Pia lipata nafasi ya kuzungumza na makundi ya vijana, viongozi ngazi ya shina hadi Wilaya wa chama na jumuiya zake, kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi katika miradi ya maendeleo ya ujenzi wa tangi la maji shule ya sekondari Moreto uliogharimu jumla ya T.sh 50 millioni, ujenzi wa kituo cha Polisi cha Lunga ambacho hadi hatua iliyofikia kinajengwa kwa nguvu za wananchi na wahisani .
Aidha alikabidhi kwa madiwani wa kata 15 wa jimbo la Chalinze cement pkt 2,287 zenye thamani ya 22,013,500/ Mabati 633 yenye thamani ya T.sh 14,559,000/ fedha taslim 5,650,000/ na fedha kwa ajili ya usafiri 3,800,000/ vilivyotolewa na Mbunge wa jimbo la Chalinze Mhe Ridhwani J. Kikwete ukiwa ni ukamilishaji wa miradi ya maendeleo ya wananchi iliyoanzishwa katika kata hizo.
*"Katika jambo kubwa la kihistori alilofanya Mhe Rais Magufuli ni kuteuwa RC, MADC, DED na DAS vijana, maeneo mengi niliyokwisha tembelea mambo yako vizuri sana, vijana wenzetu mnatuwakilisha na mnamuwakilisha Mhe Rais vilivyo tunajivunia utendaji wenu, Wilaya ya Bagamoyo na halmashauri zake zote mbili mumejipanga na mnakimbizana na kasi ya kupeleka maendeleo endelevu kwa wananchi kijamii na kiuchumi.*
*nimesikiliza taarifa ya mkuu wa wilaya na watendaji wa halmashauri kwa umakini na nimebahatika kutembelea baadhi ya miradi iliyoanzishwa na serikali na ile ya nguvu za wananchi ninyi hamna maneno mengi vitendo vya kazi ndio vingi.*
*endeleeni kulinda heshima hii ninakupongeza sana Alhaj Majid na wakurugenzi wako wote wawili, wasaidizi wenu na waheshimiwa madiwani mumejiongeza na mmekuwa wabunifu hii ndio faida ya kuwa na madiwani wote toka CCM wanaojitambua*
*nilikotembea katika maeneo mengine sijasikia wenyeviti wa vijiji wakilipwa posho kama sehemu ya kuwafanya kuongeza kazi ya kuwatumikia wananchi na kuwafanya wache kuingia katika migogoro isiyo na lazima kwa tamaa, ni kweli mkijipanga vizuri katika kusimamia mapato yenu hakuna lisilowezekana.*
*nimejionea mipango mizuri mnayoendele kuitekeleza ambayo inaonesha wazi kuwa mumedhamiria kikweli kufanya mageuzi ya kimfumo katika kuharakisha upatikanaji wa maendeleo kwa wananchi.*
*haya ndio mambo ya kuwaeleza wananchi ambayo yamefanywa na Serikali ya Chama Cha Mapinduzi ya awamu ya tano inayongozwa na Dk John Pombe Magufuli."*
Sehemu ya hotuba ya Kaimu Katibu Mkuu wakati alizungumza na viongozi wa mashina, tawi, kata, wenyeviti wa vijiji, maafisa watendaji wa vitongoji, vijiji na kata pamoja na madiwani wa kata 35 za jimbo la Chalinze na viti maalum wanawake".

Kaimu Katibu Mkuu amemaliza ziara katika Wilaya ya Bagamoyo na kesho ataendelea Wilaya ya Kibaha Vijijini.
Image may contain: 5 people, people smiling, people standing
Image may contain: 1 person, standing, sky and outdoor
Image may contain: 9 people
Image may contain: 4 people, people standing
Image may contain: 1 person

0 comments:

Post a Comment