Kamati kuu ya uongozi imekaa Imezingatia haya
Hatuna kipangamizi Rais kumteua yeyote
ACT Wazalendo ni chama cha siasa cha kutumikia wananchi
Rais kavunja mwiko kwa kuanza kuteua wapinzani
Bado tunao wazalendo wa kutosha, hivyo raia asisite kuchagua wengine
CCM wajifunze kupitia kwetu kuchagua viongozi bora
=>Kamati ya uongozi inamshauri Rais kuweka mfumo bora wa kuazima watu kutoka vyama vingine kwa kuweka mashauliano ili kuepuka migongano ndani ya vyama.Japo anao uwezo, hii ni kuimarisha umoja wa kitaifa
Kuteua bila mashauriano kunaleta wasiwasi miongoni mwao
ACT inampongeza Anna Mghwira kwa kuteuliwa
ACT imeona kutakuwa na mgongano kati ya nafasi yake na chama
Katiba ya ACT Wazalendo, Mama Anna Mgwhira amekoma kuwa mwenyekiti.
Kuteuliwa kwake kuwa Mkuu wa Mkoa hawezi fanya kazi kwa ufanisi kwa ACT- wazalendo.
ACT inamshukuru kwa kufanya kazi kwa uzalendo na ACT Wazalendo imemteua ndugu Yeremia Maganja kuwa Makamu Mwenyekiti mpya
Maswali
1. Je, hamjashauriana katika uteuzi huu?
Kama tulivyoeleza mwanzo, Rais alimteua mama wakati yupo nje ya nchi na sisi tulipata taarifa na tukamtafuta kwa mashauriano. Tumetoa tamko baada ya kushauriana na Mama Mghwira
2. Mama bado ni Mwanachama halali wa ACT Wazalendo, Kupewa ilani ya CCM mnaichukuliaje?
Rais na vitengo vyake vyote vimejilidhisha kwamba ACT ina viongozi waadilifu, huu ni ujumbe kwa watanzania kwamba ACT-Wazalendo ipo tayari kupewa nchi. Na watanzania wenyewe wameona
Ni mujimu haya mambo yakaeleweka, tunapofanya uchaguzi, wananchi wanasoma na kuchagua ilani ambayo wanaona inafaa. Kwa hivi sasa chama kinachoongoza ni CCM na ilani inayotekelezwa ni ya CCM. Mwaka 2015 Mama Anna pia alimpa ilani ya ACT Wazalendo na tunaamini kuna mambo mazuri ya Ilani ya ACT
ACT tungeshinda tungeunda serikali ya umoja wa kitaifa, hivyo hiki kinachofanywa ni moja ya Malengo tuliyokuwa nayo.ACT tungechagua watu kutoka vyama vyote

0 comments:
Post a Comment