Posted by Williammalecela.com on Friday, June 09, 2017
 |
Kamanda Sirro, Mkuu wa Jeshi la Polisi Nchini alipotembelea Rufiji majuzi na kukutana na Wananchi.
Usiku
wa kuamkia leo, watu watatu wakazi wa kijiji cha Nyamisati, wilayani
Kibiti, mkoani Pwani wameuawa kwa kupigwa risasi na watu wasiojulikana.
Taarifa ya Mkuu wa wilaya ya Kibiti, Ndg.Gullamuhusein Kifu inaeleza
kuwa miongoni mwa watu waliouawa ni mwanamke mmoja ambaye ni Mwenyekiti
wa Kitongoji kimojawapo kijijini hapo. Wengine waliouawa ni pamoja na
Hamid Kidevu, Yahaya Makame na Moshi Machela.
Ikumbukwe juzi Askari mgambo mmoja alijeruhiwa kwa kupigwa risasi akiwa shambani,
na mwingine aliuawa usiku wa siku hiyohiyo kwa kuvamiwa nyumbani kwake
na watu wasiojulikana kabla ya kupigwa risasi maeneo mbalimbali ya mwili
wake.
Mauaji haya yote
yanatolea ikiwa ni siku mbili tu tangu Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini,
IGP Simon Sirro alipofanya ziara wilayani Kibiti na kusisitiza umuhimu
wa kulinda amani na kuzuia mauaji yanayoendelea.!
|
0 comments:
Post a Comment