Saturday, June 3, 2017

ACHANA na umahiri wake awapo bungeni. Weka pembeni sauti yake ya mamlaka na wala usijishughulishe hata kidogo na ujasiri wake wa kumnaga yeyote. Joseph Kasheku ‘King Msukuma’ ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Geita Vijijini ametoa ya moyoni na kukiri urembo na ‘figa’ ya msanii Wema Sepetu haupishani na uzuri wa samaki aina ya Nguva, Ijumaa bwana teh…teh… teh…teheeeeee. Jumatatu ya wiki hii, saa saba na dakika zake mchana, mwandishi wetu akiamini King Msukuma atakuwa nje ya viunga vya bunge akiifaidi posho yake, aliamua kumtafuta kupitia simu yake ya mkononi kwa lengo la kubadilishana naye mawazo juu ya mambo mbalimbali ya kimaendeleo ndipo suala la uhusiano wake na Wema Sepetu likaibukia katikati ya mazungumzo na mbunge huyo kulitolea ufafanuzi.

TULIANZIA HAPA
Siku nne mfululizo za wiki iliyopita, mwandishi wa habari hii alimtafuta mbunge huyo kwa lengo la kufanya naye mahojiano juu ya mambo mbalimbali, ambapo alipokea simu na kusikiliza huku akimuomba mwandishi ampigie baada ya dakika tano kwa kile alichodai… “kuna kitu naweka sawa hapa…”

0 comments:

Post a Comment