Posted by Williammalecela.com on Wednesday, August 16, 2017
 |
BIASHARA
HARAMU: Kijana Sadiki wa maeneo ya Tegeta,anayedaiwa kuuza mishikaki
katika eneo lililopo karibu na jengo la Kibo Complex,
anashikiliwa na
Polisi kwa tuhuma za kuuza mishkaki ya nyama za paka.
Walaji
wengi wa mishkaki ya Sadiki walikuwa wakipatwa na mashaka na nyama hiyo
kutokana na ladha yake kuwa tofauti, lakini kila mara alipoulizwa, jamaa
huyo aliwatoa hofu kwa kuwaambia kuwa nyama hiyo ni ya ng’ombe.
Imedaiwa kutokana na mashaka ya wateja wa mishkaki hiyo kuongezeka,
wananchi wa eneo hilo waliamua kumuwekea mtego ili kubaini ukweli.
|
0 comments:
Post a Comment